Tangazo

Thursday, August 21, 2014

UKAWA WAPOTEZEWA



Katibu Mkuu wa CCM, Abrahman Kinana akitoa taarifa katika kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho, mjini Dodoma juzi. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar, Rais Ali Mohamed Shein, Rais Jakaya Kikwete na Makamu wa Tanzania Bara Phillip Mangula. Picha na Emmanuel Herman 



“Siyo lazima warejee bungeni maana hiyo siyo njia pekee ya kupatikana kwa suluhisho, kuna options (njia) nyingi za kufikia mwafaka na sisi tutazitumia hizo kwa sababu lengo letu ni kuhakikisha kwamba nchi yetu inaendelea kuwa katika hali ya usalama na amani,” alisema Kinana jana mjinihapa.
Katibu mkuu huyo alikuwa akijibu swali lililomtaka kueleza njia atakazotumia kusaka suluhu ya mchakato wa Katiba baina ya chama chake na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kama alivyoagizwa na Kamati Kuu (CC) ya CCM iliyofanyika juzi.
 
Kamati Kuu ilitoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa tatu za mwenendo wa mchakato wa Katiba zilizowalishwa na Kinana, Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa wa CCM ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Asha-Rose Migiro na Katibu wa Wabunge wa CCM na Naibu Waziri Elimu naMafunzo ya Ufundi, Janister Mhagama
.

“Kuna njia mbili kubwa za kuendelea kusaka maridhiano; kwanza ni kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na Baraza la Vyama vya Siasa ambako kuna fursa za viongozi wa vyama kujadiliana masuala mbalimbali licha ya tofauti za mitizamo na itikadi za vyama vyetu,” alisema Kinana na kuongeza:

“Tumekuwa tukizungumza na kuna kila dalili ya kupata mwafaka licha ya kwamba siyo lazima mwafaka huo uwalazimishe waliotoka kurejea bungeni, lakini jambo la msingi lazima tuhakikishe mazingira ya kuendesha siasa zetu ni salama kwa faida ya vyama vyetu nchi yetu.

Alisema mbali na suala la kuwashawishi Ukawa warejee bungeni, majadiliano ya vyama vya siasa pia yanalenga kujadili jinsi ya kujenga mazingira sawa ya uendeshaji wa siasa, hasa katika kipindi hiki Taifa linapoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Kinana alisema pamoja na kuvunjika kwa mazungumzo yaliyokuwa yakiratibiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi anaamini TCD ni sehemu mwafaka kwani inajumuisha viongozi wa vyama ambavyo siyo sehemu ya mvutano uliopo.

Taarifa za ndani

Kauli ya Kinana inashabihiana na habari kutoka ndani ya chama chake ambazo zimekuwa zikidai kwamba chama hicho tayari kimefanya mazungumzo na wapinzani kwa ajili ya kuifanyia marekebisho ya Katiba ya sasa ili kujenga mazingira ya usawa katika Uchaguzi Mkuu ujao
.

Tayari vyama vya upinzani vimependekeza mambo manne yanayopaswa kuzingatiwa katika mabadiliko hayo ambayo ni kuwapo kwa Tume Huru ya Uchaguzi, Matokeo ya urais kuhojiwa Mahakamani, kuruhusiwa kwa mgombea binafsi na mshindi wa urais kupata kura zaidi ya asilimia 50 tofauti na sasa.
Katika muktadha huo, ndiyo maana Ukawa wamekuwa na msimamo wa kutaka Bunge hilo lisitishwe kusubiri mwafaka, jambo ambalo hata hivyo, Kinana alisema ni ngumu kutekelezwa kwa sababu sheria imefunga milango kuhusu suala hilo

No comments:

Post a Comment